Tuesday, 5 May 2015

Israeli kupambana na ukatili wa polisi

Maafisa  wa  Israel  wameahidi  kupambana  na  ukatili  wa  polisi pamoja  na  ubaguzi dhidi  ya  Wayahudi  kutoka  Ethiopia. Maandamano... thumbnail 1 summary
Maafisa  wa  Israel  wameahidi  kupambana  na  ukatili  wa  polisi pamoja  na  ubaguzi dhidi  ya  Wayahudi  kutoka  Ethiopia.
Maandamano  ya  hivi  karibuni  yamezuka  baada  ya  vidio kuonesha  maafisa  wawili  wa  polisi  wakimshambulia  mwanajeshi Muisrael  mweusi  akiwa  katika  sare  za  jeshi.
Kufuatia  mkutano  na  viongozi  wa  kijamii, waziri  mkuu Benjamin Netanyahu  amesema  ubaguzi  katika  jamii  ya  Israel  ni  tatizo kubwa ambalo  linahitaji kushughulikiwa.
Ni  katika  mwaka 1984 ambapo Wayahudi  kutoka  Ethiopia waliruhusiwa kwa  mara  ya  kwanza  kuhamia nchini  Israel chini  ya sheria ya  nchi  hiyo  ya  kurejea  ambayo  inawaruhusu  Wayahudi duniani  kuwa  raia  wa  Israel. source DW

No comments

Post a Comment