Tuesday, 5 May 2015

Mtuhumiwa Texas alikuwa anachunguzwa na FBI

Kundi la Dola la Kiislamu limedai kuhusika na shambulio lake la kwanza nchini Marekani mjini  Texas  baada  ya  tukio nje ya ukumbi ulio... thumbnail 1 summary
Kundi la Dola la Kiislamu limedai kuhusika na shambulio lake la kwanza nchini Marekani mjini  Texas  baada  ya  tukio nje ya ukumbi uliokuwa na mkusanyiko  wa  watu wanaopinga  Uislamu  mjini Texas siku ya Jumapili.
Maafisa  wamefichua  kuwa  mmoja  kati  ya  watu waliouwawa  na polisi, alikuwa  anachunguzwa  kutokana na kuvutiwa  na  wapiganaji wa  Jihadi.
Watu  wawili  wamefyatua  risasi  nje  ya  kituo cha  makutano, mahali  ambapo kulikuwa  kunafanyika  shindano  la  kumchora  kwa dhihaka mtume Muhammad, shindano  lililoandaliwa  na  vuguvugu la kulinda uhuru nchini Marekani.
Kwa  mujibu  wa  dini  ya  Kiislamu, kumchora mtume Muhammad kunaonekana  kuwa  ni  kufuru. Vyombo kadhaa vya habari  nchini Marekani  vimewatambua  washambuliaji  hao  kuwa  ni Elton Simpson  mwenye  umri wa  miaka  31 na Nadir Soofi  mwenye  umri wa  miaka 34, licha  ya  kuwa  haijathibitishwa  rasmi.

No comments

Post a Comment