Wednesday, 6 May 2015
Jeshi la Kongo laishinikiza ADF
Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo liliripoti jana kwamba liliwauwa waasi 16 wa ADF, katika mapambano makali yaliyofanyika eneo hilo mwishoni mwa juma lililopita. Jeshi hilo lilianzisha mwaka jana, operesheni iliyoitwa Sukola, kwa azma ya kuwatokomeza waasi wa ADF ambao wanashutumiwa kuwauwa watu 300 katika vijiji vilivyo karibu na mji wa Beni kati ya mwezi Oktoba na Desemba. Vikosi vya Umoja wa Mataifa vililiunga mkono jeshi la Kongo katika operesheni hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments
Post a Comment