Mnamo 13 mwezi May
jenerali mmoja wa jeshi alitangaza katika redio ya taifa kwamba rais wa
Burundi amepinduliwa na kwamba serikali ya mpito itabuniwa.Lakini
msemaji wa rais alikana habari hizo akidai kuwa kulikuwa na usaidizi
mdogo katika jeshi kwa mapinduzi kutendeka.
13.30-Raia wamlaki rais Ngozi
13.23pm-Nkurunziza arudi nyumbani kwake Ngozi
12.00-Raia watakiwa kuendeleza maandamano
Vital Nshimiriman amesema kuwa licha ya kundi hilo kupinga jaribio hilo la mapinduzi,vile raia walivyowashangilia wanajeshi wa jaribio hilo kulionyesha kwamba kuna hamu kubwa ya mabadiliko.
10.30am-Majenerali waasi kushtakiwa
10.00am-Majenerali waasi wakamatwa:
Majenerali wawili waliotekeleza jaribio la mapinduzi nchini Burundi dhidi ya rais Pierre Nkurunziza wamekamatwa.
Hatahivyo kiongozi wa mapinduzi hayo jenerali Godefroid Niyombare ametoroka na anasakwa kulingana na msemaji wa rais.
Awali Jenerali Niyombare alikiambia chombo cha habari cha AFP kwamba yeye na wafuasi wake watajisalimisha akiongezea kuwa ''natumai hawatatuua''.
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amesema kuwa amerudi nchini Burund na kwamba anatarajiwa kulihutubia taifa.
bbc may
No comments
Post a Comment