Tuesday, 5 May 2015

marekani yatinga somalia, al shabab waufyata

Waziri Kerry azuru Somalia Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Marekani  John Kerry  amefanya ziara  ya  kushitukiza  nchini  Somalia  leo... thumbnail 1 summary
Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Marekani  John Kerry  amefanya ziara  ya  kushitukiza  nchini  Somalia  leo, maafisa  wamesema, akiwa  waziri  wa  kwanza  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Marekani kuzuru nchi  hiyo  ya  pembe  ya  Afrika  iliyoharibiwa  kwa  vita.
Waziri  Kerry  atakuwa  mjini  Mogadishu  kwa  saa  chache, na hakupangiwa  kutoka  nje  ya  eneo linalolindwa  la  uwanja  wa ndege ambako atakutana  na  rais  wa  Somalia Hassan Sheikh Mohamud  na  waziri  mkuu  Omar Abdirashid  Ali Sharmake.
Msemaji  wa  wizara  ya  mambo  ya  kigeni  ya  Marekani  Marie Harf  amesema  katika  taarifa  kwamba  waziri  Kerry  amewasili katika  mji  mkuu  wa  Somalia  Mogadishu, akiimarisha nia  ya Marekani kuunga mkono kipindi kuelekea demokrasia ya amani nchini Somalia.
Katika  mkutano  wake  na  maafisa  wa  serikali  kuu  na  serikali  za mikoa , atajadili  ushirikiano  wa  kiusalama na  hatua  zilizopigwa  na Somalia  kuelekea  katika  kutimiza  mageuzi na  maendeleo  nchini humo

No comments

Post a Comment