Tuesday, 5 May 2015

Madereva wa treni kugoma kwa siku 5 Ujerumani, wabongo mpaka kieleweke.

Madereva  wa  treni  wa  Ujerumani  wameanza  mgomo  wa  siku tano, ukiwa  mgomo mrefu  zaidi  katika  kile  kinachoendelea  kuwa mzozo ... thumbnail 1 summary
Madereva  wa  treni  wa  Ujerumani  wameanza  mgomo  wa  siku tano, ukiwa  mgomo mrefu  zaidi  katika  kile  kinachoendelea  kuwa mzozo  mkubwa  na  waendeshaji  wa  kampuni  ya  usafiri  wa  treni nchini  humo.
Waendesha  treni  za  abiria  wameanza  mgomo  wao  asubuhi ya leo  wakijiunga  na  waendesha  treni  za  mizigo  ambao  tayari wameanza  mgomo  wao  jana  Jumatatu.
Chama  cha  madereva  wa  treni GDL kimesema  madereva hawatarejea  kazini  hadi Jumapili  saa  tatu  asubuhi.
Kampuni  ya  usafiri wa treni  nchini Ujerumani  Deutsche Bahn, imesema  theluthi  moja  ya  treni zitaendelea kufanya kazi chini ya mpango wake  wa usaidizi.
Chama  cha  madereva  wa  treni  GDL kinataka ongezeko la asilimia 5 ya mishahara  na  muda  mfupi  wa  kazi  lakini  suala  muhimu ni madai ya majadiliano  kwa wafanyakazi wengine ikiwa  ni  pamoja na  makondakta ambao  kwa  kawaida  wanawakilishwa na chama tofauti  cha  wafanyakazi.

No comments

Post a Comment