Wakati wapigakura watakapoelekea vituoni Alhamisi wiki hii (Mei 8), wanasiasa wa nchi hiyo hawatakuwa pekee watakaosubiria matokeo ya mwisho kwa wasiwasi. Hali ya mashaka itatawala barani Ulaya kote pia, kukiwa na wasiwasi kwamba kile kinachojulikana kama "Brexit" kinakaribia.
Neno hilo lililotungwa kuelezea uwezekano wa Uingereza kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya - limekuwa likisikika mara kwa mara mjini Brussels, yaliko makao makuu ya umoja huo, tangu waziri mkuu wa Uingereza David Cameron alipoahidi kuitisha kura ya maoni juu ya uanachama wa Umoja wa Ulaya, ikiwa chama chake kitashinda uchaguzi mkuu wa mwezi huu.
Michael Emerson, kutoka kituo cha ushauri juu ya masuala yanayohusiana sera ya Ulaya, alisema uundwaji wa serikali ijayo unaweza kuwa tu mwanzo wa mashaka. " Kuondoka kwa Uingereza kunaweza kusababisha uharibifu usiyoelezeka kwa ukamilifu na uaminifu wa Umoja wa Ulaya, aliongeza mchambuzi wa kituo cha Carnage Europe Jude Dempsey, na kusema kuwa Cameron ameiweka Uingereza kwenye njia ya msuguano na washirika wake wa Ulaya, jambo alilolitaja kuwa hatari.
Kiini cha mizozo na malumbano
Lakini Cameron hajawahi kuona haya kuutikisa Umoja wa Ulaya. Katika miaka michache iliyopita, amekuwa kiini cha wasiwasi na malumbano kuhusu kila kitu, kuanzia bajeti za jumuiya hiyo, hadi kwenye nfasi za juu za ajira, uhamiaji na sheria mpya kuhusu nidhamu ya fedha. Uchunguzi wa maoni unaonyesha kuwa Waingereza ni watu wasioupenda Umoja wa Ulaya, licha ya kuwa wanachama wa jumuiya hiyo kwa zaidi ya miaka 40.. source DW. may 6, 2015
Neno hilo lililotungwa kuelezea uwezekano wa Uingereza kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya - limekuwa likisikika mara kwa mara mjini Brussels, yaliko makao makuu ya umoja huo, tangu waziri mkuu wa Uingereza David Cameron alipoahidi kuitisha kura ya maoni juu ya uanachama wa Umoja wa Ulaya, ikiwa chama chake kitashinda uchaguzi mkuu wa mwezi huu.
Michael Emerson, kutoka kituo cha ushauri juu ya masuala yanayohusiana sera ya Ulaya, alisema uundwaji wa serikali ijayo unaweza kuwa tu mwanzo wa mashaka. " Kuondoka kwa Uingereza kunaweza kusababisha uharibifu usiyoelezeka kwa ukamilifu na uaminifu wa Umoja wa Ulaya, aliongeza mchambuzi wa kituo cha Carnage Europe Jude Dempsey, na kusema kuwa Cameron ameiweka Uingereza kwenye njia ya msuguano na washirika wake wa Ulaya, jambo alilolitaja kuwa hatari.
Kiini cha mizozo na malumbano
Lakini Cameron hajawahi kuona haya kuutikisa Umoja wa Ulaya. Katika miaka michache iliyopita, amekuwa kiini cha wasiwasi na malumbano kuhusu kila kitu, kuanzia bajeti za jumuiya hiyo, hadi kwenye nfasi za juu za ajira, uhamiaji na sheria mpya kuhusu nidhamu ya fedha. Uchunguzi wa maoni unaonyesha kuwa Waingereza ni watu wasioupenda Umoja wa Ulaya, licha ya kuwa wanachama wa jumuiya hiyo kwa zaidi ya miaka 40.. source DW. may 6, 2015
No comments
Post a Comment