Monday, 4 May 2015

Wahamiaji haramu wanusurika kufa maji nchini ITALIA

Wahamiaji haramu wanusurika kufa maji nchini ITALIA Mamia ya wahamiaji haramu waliookolewa kufamaji katika bahari ya MEDIT... thumbnail 1 summary

Wahamiaji haramu wanusurika kufa maji nchini ITALIA
Mamia ya wahamiaji haramu waliookolewa kufamaji katika bahari ya MEDITERANIAN, baada ya mtumbwi waliokusa wakisafiria kuzama, wamewasili katika kisiwa cha POZZALLO, nchini ITALIA.

Walinzi katika pwani ya ITALIA wanasema katika kipindi cha saa 24 zilizopita wamewaokoa watu 877, kutoka baharini waliokuwa katika hatari ya kufa maji.

Umoja wa mataifa unasema, mwaka huu ndio unaoongoza kwa idadi kubwa ya wahamiaji haramu kuokolewa katika bahari ya MEDITERANIA, huku mamia pia wakipoteza maisha.

LIBYA, pia imeomba msaada wa kimataifa kukabiliana na wahamiaji haramu, wanaoanzia safari zao kwenda barani ULAYA, katika pwani ya nchi hiyo, kwani wahamiaji hao wanaendelea kufurika.
source; tbc

No comments

Post a Comment