Wednesday, 6 May 2015

Walimu na Wasanii watamba ligi ya UDOM, hawajafungwa tangu waanze ligi, Wanamsubiri PSPA ijumaa

Idara ya AMD imeilaza mabo 3 kwa 1 idara ya DS Chuo kiku cha Dodoma na kutamba kutinga fainali itakayochezwa saa kumi jioni ya ijumaa ta... thumbnail 1 summary

Idara ya AMD imeilaza mabo 3 kwa 1 idara ya DS Chuo kiku cha Dodoma na kutamba kutinga fainali itakayochezwa saa kumi jioni ya ijumaa tarehe 8 wiki hii. Idara ya AMD inaundwa na kozi za wasanii, wanamitindo, wanahabari, pamoja na walimu kwa asilimia kubwa. Mashabiki wa Ds waliwabeza walimu kwa kejeli kubwa huku wakisema, “ualimu ni stress, michezo hamuwezi” huku wanaidara ya AMD wakiendelea kuishabikia timu yao vilivyo na kuwapa nguvu wachezaji wake. AMD sasa inakabiliwa na kibarua kizito cha kumng’oa meno bila ganzi PSPA au wao kunyolewa bila maji siku ya kesho ili waweze kujitwalia zawadi ya ng’ombe mzima.

Zione picha za mashabiki wakiingia uwanjani na wakiwa uwanjani.










No comments

Post a Comment