Wednesday, 6 May 2015
mgomo wa madereva, makonda ajizolea ujiko
HUDUMA za usafiri wa mabasi ya mikoani na daladala, zilizokuwa zimekwama kwa saa 31 kuanzia alfajiri ya juzi, zilirejea jana mchana.
Zilirejea baada ya madereva kusitisha mgomo wao, kutokana na ushawishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda aliyezungumza nao.
Makonda pia alijitwisha mzigo wa kufuatilia madai ya madereva hao katika kamati iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ili kuona hadidu za rejea za kamati hiyo na muda wa kamati hiyo kufanya kazi.
Mkuu huyo wa wilaya alisema kwa kuwa kamati husika iliyoundwa, ina hadidu za rejea hivyo ni vyema kuzihakiki kuona kama suala la mkataba, malipo, matibabu na suala la kusoma, limo ndani ya hoja husika na kuhakiki muda husika wa Kamati kufanya kazi.
Maafikiano hayo yalitokana na kuwepo kwa mazungumzo ya muda mrefu baina ya viongozi wa madereva na wamiliki, huku Makonda na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mohammed Mpinga wakisimamia mazungumzo hayo.
Hata hivyo, madereva hao na mkuu huyo wa wilaya walikubaliana kuwa kazi hiyo isipokamilika kuanzia leo saa 4:00 asubuhi, wataendeleza mgomo huo, ambao umesababisha athari kubwa kiuchumi kwa taifa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments
Post a Comment