Maafisa wa Yemen wamesema mashambulizi hayo ya anga yamefanywa kwenye mji wa mpakani wa Najran ulio umbali wa kilomita tatu kutoka kwenye mpaka wa Yemen, baada ya waasi wa Houthi nchini Yemen kurusha makombora na roketi jana, yaliyoharibu shule moja ya wasichana na hospitali.
Hilo ni shambulizi la kwanza kufanywa na waasi hao katika eneo la Saudi Arabia, tangu muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia ulipoanzisha operesheni ya kijeshi dhidi ya waasi hao Machi 26, mwaka huu. Kwa mujibu wa maafisa hao, mashambulizi hayo ya makombora yalikuwa yakifanywa kutoka kwenye mpaka wa Saudi Arabia.
Eneo la Saada ni ngome muhimu kwa waasi wa Houthi wanaoungwa mkono na Iran. Duru za waasi hao zimeeleza kuwa raia 43 wameuawa na wengine wapatao 100 wamejeruhiwa kutokana na mashambulizi ambayo yamefanyika hadi leo alfajiri. Hata hivyo idadi hiyo bado haijathibitishwa. source bbc Swahili, mei 6 2015
Hilo ni shambulizi la kwanza kufanywa na waasi hao katika eneo la Saudi Arabia, tangu muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia ulipoanzisha operesheni ya kijeshi dhidi ya waasi hao Machi 26, mwaka huu. Kwa mujibu wa maafisa hao, mashambulizi hayo ya makombora yalikuwa yakifanywa kutoka kwenye mpaka wa Saudi Arabia.
Eneo la Saada ni ngome muhimu kwa waasi wa Houthi wanaoungwa mkono na Iran. Duru za waasi hao zimeeleza kuwa raia 43 wameuawa na wengine wapatao 100 wamejeruhiwa kutokana na mashambulizi ambayo yamefanyika hadi leo alfajiri. Hata hivyo idadi hiyo bado haijathibitishwa. source bbc Swahili, mei 6 2015
No comments
Post a Comment