Monday, 4 May 2015

UCHAGUZI CCM 2015: Mizengo Pinda Waziri Mkuu atabebwa na historia yake

WASIFU Umri:  Miaka 67 Elimu: Shahada ya Sheria (L LB) Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kazi: Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ... thumbnail 1 summary



WASIFU Umri:  Miaka 67 Elimu: Shahada ya Sheria (L LB) Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kazi: Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
Na Julius Mtatiro 
Mnamo mwaka 1995, Pinda alijaribu kugombea ubunge katika Jimbo la Mpanda Mashariki lakini alishindwa katika hatua ya kura za maoni na ikampasa kurejea kwenye kazi yake ya awali  Ikulu.

Historia yake
Mizengo Pinda alizaliwa Agosti 12, 1948 mkoani Rukwa (atafikisha miaka 67 Agosti mwaka huu).



Pinda ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu mwaka 2008.
Wazazi wa Mizengo Pinda wote walikuwa wakulima kwa hiyo kijana pia alifuata nyayo hizo huku akifanya jitihada kubwa kwenye masomo yake na kufanikiwa kuhitimu shule ya msingi na sekondari, akifaulu vizuri kila alikopita.
Baada ya masomo yake ya sekondari, Pinda alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kusomea Shahada ya Sheria (LLB) mwaka 1971 hadi 1974. Baada ya kuhitimu, alijiunga katika utumishi kwenye Wizara ya Sheria akiwa Mwanasheria wa Serikali na alikaa katika utumishi huo tangu mwaka 1974 hadi 1978.
Mwaka 1978, alifanya kazi akiwa “Ofisa Usalama wa Taifa” akiwa Ikulu hadi mwaka 1982, Rais wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere alipomteua kuwa katibu wake binafsi (Katibu wa Rais) nafasi aliyoishikilia hadi mwaka 1985.
Baada ya Mwalimu Nyerere kung’atuka na kuikabidhi nchi kwa Ali Hassan Mwinyi, Pinda alitakiwa kubaki kuendelea kumsaidia Mzee Mwinyi na alikubali wito huo. Akaendelea kuitumikia Ikulu chini ya utawala wa Mwinyi hadi mwaka 1992.
Mnamo mwaka 1995, Pinda alijaribu kugombea ubunge katika Jimbo la Mpanda Mashariki lakini alishindwa katika hatua ya kura za maoni na ikampasa kurejea kwenye kazi yake ya awali  Ikulu.
Baada ya Mkapa kuteuliwa kurithi Ikulu mwaka 1995, alimteua Pinda kuwa karani wa Baraza la Mawaziri. Wadhifa alioushikilia kuanzia mwaka 1996 hadi 2000.
Pinda amemuoa Tunu na wamepata watoto wanne; Janet, Jenifer, Hardwick na Narusi.
Mbio za ubunge
Mwaka 2000, Pinda aliachana na utumishi ndani ya Serikali na Ikulu akajitupa jimboni Katavi kusaka ubunge kwa mara nyingine, safari hii alipita ndani ya kura za maoni za CCM akafanikiwa kuwashinda wapinzani na kuwa mbunge.
Nyota ya Pinda ilizidi kung’ara mwaka 2001, pale Rais Mkapa alipomteua kuwa Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) akifanya kazi chini ya waziri wake, Brigedia Jenerali Hassan Ngwilizi, hadi mwaka 2005.

No comments

Post a Comment